Msaada wa jamii - Namna ya kuhakikisha ufuatiliaji wa waliookoka katika ukatili wa kijinsia

Kiisha  mashauri ya kwanza, lazima yule yule aliye kumbwa na vitendo vya uwaki arudi kwa munganga  ndani ya muda unayowekwa hapa chini lakini pia ndani ya mipango  ya APS:

 Hakikisha ufuatiliaji huku ukiheshimu mwendo, mahitaji yanayofaa pamoja na tarehe za mwisho zinazohitajika kwa kila kesi:

a. Wiki 2 baada ya matibabu ndani ya masaa 72:

Msaada wa jamii unapaswa kufanya nini miezi 3 baada ya yule aliye kumbwa na uwaki kuondoka kwenye kituo cha afya:

  • Fuatilia ikiwa mwaziriwa  alirudi kweli  kwenye kituo cha afya
  • Kucungaza kama kweli mwaziiriwa alitumia dawa kama vile inaitajika. 
  •  Kucunguza kama hakuna shida mwaziiriwa alipata kupitiya kutumiya dawa.

b. Mwezi wa kwanza kisha matibabu ndani ya masaa 72.

Msaada wa jamii unapaswa kufanya nini wiki 4 baada ya mwazirika kuondoka kwenye kituo cha afya

  •  Fuatilia ikiwa mwaziriwa alirudi kweli  kwenye kituo cha afya
  •  Kucungaza kama kweli mwaziriwa alitumia dawa kama vile inaitajika. 
  • Kucunguza kama hakuna shida mwaziiriwa alipata kupitiya kutumiya dawa.
  •  Ku harifu APS kuusu ujiyo wa mwaziiriwa kwenye kituo cha afya.

c.  Mwezi wa 3 kisha matibabu ndani ya ma saa 72.:

Msaada wa jamii unapaswa kufanya nini myezi 3  baada ya mwazirika kuondoka kwenye kituo cha afya:

  • Fuatilia ikiwa mwathiriwa alirudi kweli  kwenye kituo cha afya
  • Kusikiliza mwathiriwa kama anaweza kuwa na shida ingine
  • Ku harifu APS kuusu kufika kwa mwathiriwa kwa mafunzo ya Afya.

d. Katika mwezi wa 6 baada ya matibabu ndani ya masaa 72:

Msaada wa jamii unapaswa kufanya nini miezi 6 baada ya mwazirika kuondoka kwenye kituo cha afya

  •  Fuatilia ikiwa mwathiriwa amerejea kwenye kituo cha afya
  •  Msikilize aliyenusurika. ikiwa kuna shida nyingine. 
  •  Mwishoni ripoti APS ya kuwasili kwa mwathirika katika kituo cha afya.

e. Au Katika mwezi wa 12 baada ya matibabu ndani ya masaa 72:

Msaada wa jamii unapaswa kufanya nini miezi 12 baada ya mwathirika kuondoka kwenye kituo cha afya: 

  • Fuatilia ikiwa mwaziriwa amerejea kwenye kituo cha afya
  • Msikilize aliye pitiya vitendo vya uwaki. ikiwa kuna shida nyingine. 
  • Mwishoni ripoti APS juu ya kufika  ya aliyeokoka  ku  kituo cha afya.
    Wakati wowote mwazirika anapokuja kukutana na msaidizi wa jamii,  Nini cha kufanya na mtazamo wa kuchukua

Nini cha kufanya  :

  • Kumkaribisha aliye tendewa uwaki. 
  • Jitambulishe tena
  • Hakikisha kama  kuko burafiki  bwa karibu. 
  • Hakikisha kama ni salama  kwa aliyeokoka  kuzungumza nawe kwa wakati huu
  • Sema  kazi yako yenye  ni kuelewa shida yao ya sasa na kuchungu umuhimu  wa kuongoza kwenye  kituo ca  afya.
  • Eleza yanao angaliya  usiri na mipaka yake
  • Eleza haki zao (mnusurika anaweza kuacha, kukataa kujibu, kuuliza maswali) 
  • Eleza jinsi habari zitachungiwa 
  • Muulize kama ana maulizo  yoyote
  • Muombe ruhusa  ya kuendelea

Mtazamo

Kueshimiya kanuni zenye zinaongoza:

  • Haki ya usiri. Maelezo ya aliyeokoka  haisemeki  bila ruhusa 
  • Haki ya usalama: Usalama wa kimwili na kihisia ya aliye okoka  lazima uhakikishwe wakati wote wa usaidizi
  • Haki ya utu na kujitawala: Maoni na maamuzi ya mtu aliyeokoka  yanaheshimiwa na kufuatwa  kwa vile vilivyo. 
  •  Kutobagua: Kila aliyeokoka  hupokea matibabu na huduma sawa
  • Hali ya sura yenye inafaa.
  • Onyesha sura ya furaha.
  • Sauti  ya upole
  • Onyesha mambo mengine ya asili..
  • kama  ni mtoto, ji shushe mpaka ku kimo yake.
  • Mutege sikiyo  (usipokee simu, n.k.) 
  • Usimkate wakati iko nasema; mpe muda wa kuongea
  • Tumikisha luga ya heshima
  • Usilaganishe byenye hauta weza kufanya. 
  • Sema habari ya kweli na ya ku aminika
  • Fuata: fanya kile unachosema utafanya
  • Usimwambie mtu kile “anachopaswa” kufanya, na mpe taarifa za kumsaidia kufanya byenye  anakusudiya yee  peke.